Thursday, July 31, 2014

SIKILIZA RIPOTI YA HALI YA HAKI ZA BINADAMU KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA JANUARI – JUNI 2014



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - HALI YA HAKI ZA BINADAMU KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA
JANUARI – JUNI 2014

Ndugu waandishi wa habari
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, kinaendeleza utaratibu wake wa kila mwaka wa kutoa tathmini ya hali ya haki za binadamu kwa kipindi cha miezi sita. Tathmini hii hufanywa kwa malengo ya kutoa muelekeo wa hali ya ulinzi na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Taarifa hizi ni matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanywa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, ufuatiliaji wa ukiukwaji wa haki za binadamu, pia taarifa mbali mbali toka kwa waangalizi wa haki za binadamu, wasaidizi wa kisheria, taarifa rasmi toka taasisi za Serikali, Bunge, Mahakama, vyombo vya habari na asasi mbali mbali zisizo za kiserikali.

Wednesday, July 30, 2014

SIKILIZA KIPINDI CHA MLINZI WA HAKI - Kuchambua Sura ya Kwanza Mambo ambayo Hayakuguswa na Bunge la Katiba

WASIKILIZE



Prof Paramagamba akielezea asili ya  jina la Tanzania



HAROLD SUNGUSIA akidadavua neno nchi





Mwal hayati Nyerere alihamasisha ulinzi wa katiba
Prof Ruth Meena achambua  Tunu za Taifa, Watu na Ardhi


Dr.Aidani Msafiri anachambua  Tunu za Taifa, Watu na Ardhi na
Shehe  Mustafa Rajabu akifafanua Ukuu na utii wa katiba


Monday, July 28, 2014

WANANCHI WAELIMISHWE ELIMU YA URAI NA KATIBA - SIKILIZA Mlinzi wa Haki

SIKILIZA MDAHALO - NI NANI ANAKWAMISHA KUPATIKANA KATIBA MPYA TANZANIA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Stephen Wassira akiwakilisha CCM, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, jana walitoana jasho katika mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na East African Business and Media Institute.


Mdahalo huo uliohudhuriwa na watazamaji wapatao 500, ulikuwa na mada inayosema: ‘Nani anakwamisha Upatikanaji wa Katiba Mpya.’ Kila upande ulitumia fursa hiyo kutupa shutuma kwa mwingine huku jazba na kelele vikitawala miongoni mwa waliohudhuria.

Wednesday, July 16, 2014

Maoni ya Wananchi kurejea tena Bunge la katiba Mwezi Agosti

Mwezi Agosti ni mwezi unaotazamwa na kila jicho la Mtanzania kama Mwezi wa Mwanzo mpya wa Upatikanaji wa Katiba Mpya Ya Tanzania. Je Wananchi wana mtazamo gani? Sikiliza Makala Hii.

Monday, July 14, 2014

SIKILIZA mtazamo wa jamii juu ya Unyanyasaji katika Ndoa



Jamii inamtazamo gani juu ya Ndoa? Je Ndoa ni kitu cha kuvumilia hata pale kunapokuwa na ukatili? Sikiliza Mtazamo wa wakongwe.
Kila jumanne kutoka
Redio One Stereo
MLINZI WA HAKI