TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI - HALI YA HAKI ZA BINADAMU KWA KIPINDI CHA
NUSU MWAKA
JANUARI
– JUNI 2014
Ndugu
waandishi wa habari
Kituo
cha Sheria na Haki za Binadamu, kinaendeleza utaratibu wake wa kila
mwaka wa kutoa tathmini ya hali ya haki za binadamu kwa kipindi cha
miezi sita. Tathmini hii hufanywa kwa malengo ya kutoa muelekeo wa
hali ya ulinzi na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Taarifa
hizi ni matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanywa na Kituo cha Sheria
na Haki za Binadamu, ufuatiliaji wa ukiukwaji wa haki za binadamu,
pia taarifa mbali mbali toka kwa waangalizi wa haki za binadamu,
wasaidizi wa kisheria, taarifa rasmi toka taasisi za Serikali, Bunge,
Mahakama, vyombo vya habari na asasi mbali mbali zisizo za
kiserikali.
Katika
kipindi cha miezi sita, tathmini ya hali ya haki za binadamu
imezingatia hali halisi ya tabia na hali ya watu kwa mujibu wa sensa
ya watu na makazi ya mwaka 2012 kama ilivyotolewa na mtakwimu mkuu.
Takwimu za sensa ya watu na makazi inaonyesha wanawake kuwa wengi
kuliko wanaume, idadi ya wanawake ni asilimia 51.3 na wanaume ni
asilimia 48.7. Lakini bado idadi ya wanawake katika vyombo mbalimbali
vya maamuzi na fursa nyinginezo mbalimbali bado ipo chini
ukilinganisha na wanaume. Bado mwanamke ni mhanga mkubwa wa vitendo
vya ukatili wa majumbani na ubakaji kama takwimu za nusu mwaka
zinavyosema, mpaka kufikia Juni mwaka huu 2014 wanawake na wasichana
2878 walibakwa, vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na wasichana
vile vilivyoripotiwa polisi nchi nzima vilikuwa 3,633.
Taarifa
hii ya sensa ya watu na makazi pia inaonyesha kwamba, idadi kubwa ya
watu wanaishi vijijini. Licha ya kuwa na idadi kubwa ya wananchi
wanaoishi vijijini bado huduma za jamii kama upatikanaji wa maji,
huduma za afya, shule pamoja na umeme vijijini ni duni. Takwimu
zinaonesha, bado vijijini kuna makazi duni ya wananchi kutoka na
gharama kubwa za saruji na vifaa vya ujenzi. Mfano katika suala la
upatikanaji maji makazi 3,959,857 yanatumia vyanzo vya maji visivyo
salama ukilinganisha na makazi 1,902,244 yanayotumia maji ya bomba
nchi nzima.
Idadi
ya wananchi wengi wapatao 11,359,090 wanategemea kilimo kama shughuli
kuu ya uchumi. Hata hivyo wakulima wengi bado wanatumia jembe la
mkono. Uwekezaji katika mashamba makubwa wamepewa wawekezaji wakubwa,
Mfano: Mashamba makubwa ya Mpunga yaliyokuwa ya shirika la NAFCO huko
wilayani Mbarali-Mbeya wamepewa wawekezaji na wakulima wazawa
wametengewa maeneo yasiyofaa. Hii huchochea migogoro ya mara kwa mara
ya ardhi katika wilaya hiyo ya Mbarali.
Kiwango
cha Elimu bado kipo chini sana katika nchi. Kwa mujibu wa sensa ya
watu na makazi idadi ya watanzania waliopata elimu rasmi ni watu
14,495,447. Kati yao watu 11,848,323 wamehitimu elimu ya msingi na
wenye elimu ya chuo kikuu ni watu 337,881 tu. Hii ni changamoto kubwa
katika kulinda na kuheshimu haki za binadamu. Tafiti zetu mbalimbali
zimeonyesha kwamba ongezeko kubwa la watu kujichukulia Sheria
mikononi, mauaji yanayotakana na imani za kishirikina, mauji ya watu
wenye ulemavu wa ngozi ni matokeo ya uelewa mdogo wa wananchi juu ya
haki za binadamu. Pia zinachangiwa na kukoseka kwa elimu ya haki za
binadamu katika mifumo yetu ya elimu. Kwa mfano kwa kipindi cha nusu
mwaka watu 320 wameuawa kwa imani za kishirikina ukilinganisha na
watu 303 kwa kipindi kama hiki mwaka 2013. Hii inaonesha kuna
ongezeko la matukio haya, idadi ya watu waliouawa na wananchi
wanaojiita wenye hasira kali matukio 473 yameripotiwa ukilinganisha
na matukio 597 mwaka 2013 ambapo kitakwimu inaonesha kupungua,
matukio ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yameanza kuongezeka
pia kwa kipindi cha miezi sita iliyopita ambapo watu 2 wameripotiwa
kuuawa na wengine kujeruhiwa vibaya.
Wananchi
kuvamia vituo vya polisi na kusababisha vifo na hasara kubwa ya mali
pia matukio haya yameendelea kuripotiwa ambapo kwa kipindi cha miezi
sita vituo vitatu vya polisi vilivamiwa na wananchi na kusababisha
vifo kwa askari 2 na mgambo 1. Pia jumla ya askari sita waliouawa
katika matukio ya uhalifu.
Matukio
ya ajali za barabarani yameendelea kutokea kutokana na sababu
mbalimbali ikiwemo ubovu wa vyombo vya usafiri, miundo mbinu mibovu,
na uzembe wa watumiaji wa barabara. Kwa mwaka huu 2014 katika kipindi
cha miezi sita watu 1505 walipoteza uhai (Wanaume 1292 na wanawake
213).
Haki
ya kuwa na familia ni moja ya haki za binadamu. Takwimu za sensa ya
watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kwamba jumla ya watu
12,570,491 wameoa na kuolewa, 8,730,828 hajaoa wala kuolewa, watu
1,578,568 wanaishi pamoja, watu 232,415 wametengana, watu 715,447
wameachana, wajane 765,284 na yatima ni 1,696,349. Takwimu hizi
zinatuelekeza kuna wajibu mkubwa sana wa kulinda na kuheshimu haki
hii ya kuwa na familia bora. Katika kipindi cha miezi sita tumeona
matukio mengi ya kikatili dhidi ya wanafamilia katika matukio
mbalimbali dhidi ya watoto na wanawake. Mfano: Matukio ya kikatili
dhidi ya wanawake yanayohusiana na mahusiano ya kimapenzi Mbeya peke
yake wanawake 26 waliuawa katika mahusiano haya, pia mauaji
yaliyodumu kwa muda huko Butiama suala la mahusiano pia linatajwa
kama moja ya sababu ambapo watu 10 waliuawa. Huko Geita wanawake 27
wameripotiwa kuuawa katika matukio ya namna hiyo.
Matukio
ya ukatili dhidi ya watoto yameripotiwa kwa kiwango kikubwa, ikiwa ni
pamoja na kuibuliwa kwa watoto wanaofanyiwa ukatili na kufichwa ndani
kama ilivyotokea kwa mtoto wa mmoja mkoani Morogoro ambaye alifariki
siku chache baadaye.
Haki
ya kuishi katika mazingira safi na salama ni changamoto kubwa ambayo
inachochewa na uharibifu mkubwa wa mazingira unaosababishwa na
shughuli za binadamu. Mfano bado idadi kubwa ya kaya Tanzania
zinatumia nishati ya kuni kwa kupikia. Takwimu za watu na makazi
zinaonyesha kwamba, kaya 6,353,229 wanatumia kuni, kaya 2,381,837
wanatumia mkaa, na wale wanaotumia nishati mbadala kama mafuta ya taa
ni kaya 225,270, umeme 158,987 tu. Hivyo basi ipo haja ya Serikali
kupunguza kodi na kuhimiza matumizi ya nishati mbadala ili kulinda na
kuhifadhi misitu yetu
Migogoro
ya ardhi, Tafiti ndogo juu ya migogoro ya ardhi nchi inaonyesha kuna
changamoto nyingi za ardhi nchini. Utafiti katika wilaya mbali mbali
zilizotembelewa kama vile Mvomero, Kilosa, Kilombero, Mbarali,
Kyerwa, Karagwe, Misenyi, Babati na Kiteto inaonyesha bado kuna
changamoto kubwa juu ya umiliki, usimamizi na matumizi ya ardhi.
Migogoro hii ni baina ya wawekezaji na wananchi, wafugaji na
wakulima, wananchi na Serikali pia wilaya na wilaya mfano wilaya ya
Longido na Arumeru vijijini vinavyopakana vimekuwa na migogoro ya
mipaka ya mara kwa mara. Migogoro hii hupelekea maafa kwa jamii na
kwa taifa kwa ujumla, mfano wilayani Kiteto mwanzoni mwa mwaka 2014
yalipotokea mapigano makali na kusababisha vifo na uharibifu mkubwa
wa mali.
Usimamizi
na utoaji haki, bado kuna changamoto kubwa, mfano idadi ya majaji wa
mahakama ya Rufani bado ni ndogo ukilinganisha na idadi ya kesi kwa
mwaka. Kwa sasa mahakama ya rufani ina majaji 16 tu, na mahakama kuu
ina majaji 69. Idadi hii bado ni ndogo ukilinganisha na idadi ya
watumia huduma za mahakama. Katika mahakama za wilaya na mahakama za
mwanzo idadi ya mahakimu ni ndogo pia ukilinganisha na idadi ya
mahakama zilizopo nchi nzima. Idadi ya mahakimu kwa sasa ni 672
wakati mahakama za mwanzo pekee ni 960.
Hali
ya uchakavu wa Mahakama nyingi za mwanzo ni tatizo linalochelewesha
utoaji haki na linaongeza gharama za uendeshaji wa mashauri
mbalimbali hususani ya jinai. Mfano kati ya mahakama 960 mahakama 803
ndizo zinazofanya kazi na mahakama 157 ni chakavu. Pia mahakama 487
tu ndio zenye mahakimu wa kudumu (wakazi wa eneo la mahakama) na
mahakama 316 zina mahakimu wanaotembelea na mahakimu mara moja au
mbili kwa wiki. Ili kulinda na kutoa haki ipo haja ya Serikali
kuimarisha mifumo ya utoaji haki na utawala wa Sheria kama haki ya
Kikatiba chini ya Ibara ya 13 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, 1977.
Taarifa
hii pia imeonyesha changamoto mbalimbali za haki za binadamu ikiwa ni
pamoja na hali ya rushwa, elimu, na haki ya kupata maji safi na
salama; Hivyo basi Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu Kinapendekeza
yafuatayo
- Elimu ya Haki za Binadamu inapaswa kujumuishwa kwenye mfumo wa elimu rasmi wa nchi ili kuweza kukuza uelewa wa haki za binadamu
- Serikali inatakiwa kutekeleza mpango wa kitaifa wa haki za binadamu ikishirikiana na wadau wengine kama asasi zisizo za kiserikali na vyombo vya habari
- Tunaitaka Serikali kutunga Sheria inayolinda haki za mtoa taarifa ili kuweza kupata ushirikiano wa wananchi katika mapambano dhidi ya rushwa
- Tunaitaka serikali kutoa kipaumbele katika kuboresha upatikanaji wa huduma za jamii kama vile maji, umeme, elimu, na afya.
- Kuboresha mifumo ya utoaji haki kwa maana mahakama na mabaraza mbali mbali ya utatuzi wa migogoro ili kukuza dhana ya utawala wa sheria
- Haki ya kuishi imeonekana ni moja ya haki zinazokiukwa kwa kiwango kikubwa hivyo basi ipo haja ya wadau mbali mbali ikiwa ni pamoja na viongozi wa dini kuiasa jamii kuheshimu haki ya kuishi
- Haki za watoto na wanawake ipo haja kwa jamii yetu kulinda na kuheshimu haki hizi za makundi haya muhimu katika jamii ili tuweze kukuza ustawi na maendeleo ya taifa.
Mwisho
ninawatakia kila la heri katika harakati na kazi za kueneza na kukuza
uelewa wa haki za binadamu na utawala bora ili tuweze kufikia jamii
tunayotaamali ya haki na usawa.
Nawashuruku
sana kwa kunisikiliza na ushirikiano
Dr.
Helen Kijo-Bisimba
Mkurugenzi
Mtendaji - LHRC
No comments:
Post a Comment